Meli ya LCT Spice Islanders ikiwa imezama pwani ya Nungwi katika bahari ya Hindi Kaskazini Unguja ilipokuwa ikielekea Kisiwani Pemba ikiwa imebeba abiria wapatao 610 pamoja na mizigo usiku wa kuamkia leo.
Baadhi ya wanajeshi wa kikosi cha jeshi la polisi (FFU) pamoja na wnaharakati wengine wa uokozi wakibeba majeruhi aliyenusurika na kifo katika ajali ya kuzama kwa meli ya Mv Spice Islanders katika ufukwe wa bahari ya Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, akiwafariji majeruhi wa tukio la kuzama kwa meli ya Mv Spice Islanders katika ufukwe wa bahari ya Nungwi mkoa wa Kaskazini
.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein, akimfariji Ramadhan Haji, mkaazi wa Saateni Mjini Unguja, majeruhi wa tukio la kuzama kwa meli ya Mv Spice Islanders katika ufukwe wa bahari ya Nungwi, mkoa wa Kaskazini Unguja
Baadhi ya wananchi wakiwa katika viwanja vya Hospitali ya Mnazi Mmoja kusubiri maiti za jamaa zao waliokufa katika ajali ya meli iliyozama ya Mv Spice Islanders huko Nungwi mkoa wa Kaskazini Unguja.
Basi kama wanavyoonekana godoro au fridge au Mungu lakini wameokoka hivyo
Basi Mungu ni mkubwa hawa jamaa sijui walikaa kwa muda gani mpaka hiyo sea bus ilipowasili.
Vyanzo:TZMPAKAAU,IPPMEDIA,Zanzibar yetu,na picha nyingi kwa hisani ya Othman Ramadhani
Keine Kommentare:
Kommentar veröffentlichen