Best Blogger TipsSoon

Samstag, 25. Juni 2011

TZMPAKAAU

   Hörst Kholer ashangaa uharaka wa sarafu ya pamoja ya EAC
  • Ashauri maoni ya wananchi yasikilizwe na yazingatiwe
  • Asema EAC ijifunze toka EU(European Union) iliyochukua miaka 10 kuwa na Euro

Rais wa zamani wa ujerumani Hörst Kholer

Profesa Kohler aliyasema hayo, wiki iliyopita, mjini Arusha, kwenye mdahalo maalumuwa kuangalia Matarajio na Uhalisia wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) katika Ulimwengu wa Utandawazi. Mdahalo huo ulihudhuriwa na watu mbalimbali maarufu wakiwemo wanadiplomasia kadhaa.

Rais huyo wa zamani wa ujerumani ambaye pia ni mtaalamu wa uchumi na mwanasiasa wa Christlich Demokratische Union(CDU) cha ujerumani, ameeleza kushangazwa kwake na haraka inayoonekana katika kuzifanya nchi za Afrika Mashariki kuwa na sarafu ya pamoja. Amesema kwamba jambo hilo ni nyeti na linahitaji muda mrefu zaidi wa wananchi wanchi hizo kushauriana na kujadiliana kabla ya uamuzi wa kuwanayo haujafikiwa.

“Kwa nini kuna haraka katika jambo la msingi na muhimu kama hili?alihoji

 Proffesa Kholer anayasema haya wakati baadhi ya nchi wanachama wa E.U zikikabiliwa na matatizo makubwa kufuatia sarafu ya pamoja ya EURO nchi hizo ni kama Ugiriki,Spain na Ireland.

E.A.C(East African Community)

Kwa habari zaidi  http://www.raiamwema.co.tz/rais-wa-zamani-ujerumani-ashangaa-uharaka-wa-sarafu-ya-pamoja-eac

Keine Kommentare:

Kommentar veröffentlichen