Wachina wengi wanaishi kwa msemo huu"Mazuri yao tuyaige...". Na hii ni siri kubwa sana katika mafanikio ya Watu wa jamhuri ya uchina na majirani zao. Kama uthibitisho
Kijana huyu wa kichina ambaye ni kinyozi na mwanamitindo ya nywele ameanza kutengeneza gari yake aina ya Lamborghini Reventon.Kijana Asan kutoka mji wa Kunming jimbo la Yunan nchini China anasema Lamborghini Reventon ni gari nzuri lakini bei yake ipo juu sana hivyo ameamua kuiga mtindo wa gari hiyo na kutengeneza Lamborghini yake mwenyewe,kutumia gari yake ya mwaka 1995 aina ya Nissan CefiroA31.Anakadiria atatumia dola 14,000 tu kukamilisha ndoto yake .
Hii ni Lamborghini Reventon halisi .
Huyu ndo jamaa anakomaa kukamilisha ishu yake
Lamborghini Reventon halisi ikiwa imefunguliwa milango yake
Kijana Asan anasema milango sio kazi labda waseme kingine
Kama hiyo haitoshi kuna kundi moja la Orchesta la watu wa jamhuri ya uchina wameweza kuuimba vizuri kabisa mwimbo wa Malaika, wimbo ambao umepata umaarufu mkubwa na kuimbwa na kurekodiwa mara kwa mara na wanamuziki mbalimbali ikiwajumuisha Boney M.
sasa swali ni je wewe unaiga mazuri ya wenzako au...?
Keine Kommentare:
Kommentar veröffentlichen