Gbagbo azingirwa na majeshi ya mpinzani wake
Mji mkuu wa biashara wa Ivory Coast umezingirwa na wapiganaji wanaomunga mkono kiongozi anaetambuliwa na Jumiya ya kimataifa Alassane Outtara.
Rais Gbagbo aliyepo madarakani
Bw Outtara alitoa taarifa Alhamisi jioni akieleza kwamba vikosi vinavyomunga mkono, vimewasili nje ya Abidjan, na ametoa wito kwa wapiganaji watiifu na Gbagbo kujisalimisha. Washauri wake wanatabiri kwamba itachukuwa muda wa masaa kadhaa kabla ya Bw Gbagbo kuondolewa madarakani.Na taarifa zilizotufikia zinaeleza wanajeshi watiifu wa Alassane Outtara wameshaanza kuelekea katikati ya mji mkuu Abdijan kufanya mapambano wanayoyaita ya mwisho ya kuung`oa utawala wa bw Gbagbo.
Vyanzo:telegraph,TZMPAKAAU,voanews
Keine Kommentare:
Kommentar veröffentlichen