Mchezaji wa timu ya Taifa ya Rwanda (Amavubi) na timu ya Simba Patrick Mutesa Mafisango (32), amefariki dunia jana alfajiri kwa ajali ya gari.Amepata ajali hiyo akitokea kwenye Ukumbi wa Starehe wa Club Maisha uliyopo Masaki. Akizungumza Dar es Salaam leo, Makamu Mwenyekiti wa klabu ya Simba Geofrey Nyange Kaburu, alisema Mafisango alikubwa na mauti hayo eneo la Keko jirani na Chuo cha VETA jijini Dar es Salaam.Alisema Mafisango amekufa kwa ajali ya gari, baada ya gari alilokuwa anaendesha kuacha njia na kugonga mti ulio pembezoni mwa barabara ya Chang’ombe majira ya saa kumi kasorobo alfajiri na kufariki papo hapo.
Gari aina ya toyota cresta aliyopata nayo ajali marehemu Patrick Mafisango.
Watu wengi walikuwepo leaders kuuaga mwili wa marehemu Patrick Mafisango hawa ni makocha wa Taifa stars.
Msiba wa Mafisango uko katika eneo la Keko Toroli jirani na kituo cha Chang’ombe Maduka Mawili eneo la njia Panda ya Sigara.Mwili wa marehemu unatarajiwa kuagwa Ijumaa saa nne asubuhi katika viwanja vya Leaders, Kinondoni jijini Dar es Salaam kabla ya mwili wakekusafirishwa kwenda Kinshasa majira ya saa kumi jioni.Vyanzo:TZMPAKAAU , The Habari,Global Publishers na in2eastafrica
Keine Kommentare:
Kommentar veröffentlichen