Best Blogger TipsSoon

Mittwoch, 15. Februar 2012

TZMPAKAAU

KUJIUZULU KWA DK.MPONDA BADO NI KITENDAWILI
(RESIGNATION OF MINISTER HADJI MPONDA STILL DOUBTFUL)
Waziri wa Afya na ustawi wa Jamii Dk.Hadji Mponda.
(Minister of Health and Social Welfare Dk.Hadji Mponda)
Hatma ya Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hadji Mponda, ambaye anashinikizwa ajiuzulu kutokana na kuboronga mambo katika kushughulikia mgomo wa madaktari, bado ni kitendawili.
Kushoto ni Rais Jakaya Mrisho Kikwete na kulia ni katibu mkuu ikulu Peter Alanambula Ilomo.

Katibu Mkuu wa Ikulu, Peter Alanambula Ilomo, alisema suala la kuchukuliwa hatua za kuwajibishwa Dk. Mponda na Naibu wake, Dk. Lucy Nkya, kutokana na mgomo wa madaktari, lipo juu ya uwezo wake hivyo hawezi kulitolea maelezo kama Rais Jakaya Kikwete amechukua uamuzi gani hadi sasa dhidi ya viongozi hao.
“Mimi ni Katibu Mkuu Ikulu, lakini katika suala la Waziri wa Afya na Naibu wake, angeulizwa Katibu Mkuu Kiongozi, yeye ndiye anaweza kujua kama Mheshimiwa Rais amechukua hatua gani".
Vyanzo:TZMPAKAAU,Ippmedia na Swahilivilla

Keine Kommentare:

Kommentar veröffentlichen