Best Blogger TipsSoon

Dienstag, 6. September 2011

TZMPAKAAU

 Magufuli sasa aivunja kamati ya manunuzi ya Tanroads
  • Asema inanuka rushwa na inaiingizia serikali hasara
Waziri wa ujenzi ndg J.P.Magufuli

Waziri wa Ujenzi, Dk. John  Magufuli, amesema Kitengo cha Manunuzi makao makuu ya Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) kinanuka kwa rushwa na kutangaza kukivunja kwa maelezo kuwa kinaendelea kuitia hasara serikali.

Dk. Magufuli alitangaza hatua hiyo jana jijini Dar es Salaam wakati mkutano wa wakandarasi uliofunguliwa na Rais Jakaya Kikwete.
Alisema watumishi wa kitengo hicho wanaongeza gharama katika miradi ya ujenzi na kuongeza kwamba hivi sasa kilomita moja ya barabara inajengwa kwa Sh. bilioni 1.8 huku barabara ikiwa chini ya kiwango.

“Mheshimiwa Rais, lazima kuwepo na nidhamu katika matumizi ya fedha za serikali ili ziendane na miradi husika na sio vinginevyo,” alisema waziri Pombe Magufuli.

Waziri Magufuli anayeonekana mbele kabisa akikagua mradi mmojawapo wa barabara

Alisema serikali imedhamiria kwa dhati kuboresha sekta ya barabara nchini na kuongeza kuwa mwaka 2011/2012 wizara yake imetengewa Sh. trilioni 1.49 na kwamba fedha hizo zitaishia kwenye ujenzi wa barabara.

Huku akishangiliwa na washiriki wa mkutano huo, Dk. Magufuli alianza kutaja miradi mbalimbali ya barabara, sehemu ilipo na kila moja kuanisha inajengwa kwa kilomita ngapi.

Vyanzo :TZMPAKAAU,IPPMEDIA

Keine Kommentare:

Kommentar veröffentlichen