Best Blogger TipsSoon

Donnerstag, 4. August 2011

TZMPAKAAU

 

Umoja wa mataifa wa laani Syria

 

Baraza la usalama la umoja wa mataifa kwa mara ya kwanza limetoa taarifa inayolaani ukiukaji wa haki za binadamu nchini Syria.

Rais wa Syria Bw.Bashar Al Assad na mke wake



Kauli hiyo imetolewa miezi kadhaa baada ya mashauriano ya kina ambayo yalikuwa yamesababisha migawanyiko kwenye baraza hilo kuhusu matukio nchini humo.
Hata hivyo Lebanon imesitakuunga mkoto taarifa hiyo rasmi.
Taarifa hiyo haijatosheleza matakwa ya nchi za ulaya lakini hata hivyo imekuwa na uzito kando na ilivyo tarajiwa.
Hata hivyo baraza hilo limesisitiza kuwa suluhu ya mzozo unaoendelea nchini humo itapatikana kupitia machakato wa kisiasa utakaoongozwa na raia wa syria wenyewe.
 
Waandamanaji wa Syria wakimuombolezea mwenzao aliyeuawa na majeshi ya serikali ya Damascasi

Kauli hiyo imezima matumaini kuwa dola za kigeni zitaingilia kati mzozo unaoenedlea nchini humo.
Wanadiplomasia wanasema taarifa hiyo rasmi ya baraza la usalama ni onyo kwa utawala mjini Damascas.
Lakini Lebanon, hawajaunga mkono taarifa hiyo, suala ambalo halikutarajiwa ukizingatia ushawishi mkubwa wa Syria nchini humo.

Vyanzo:TZMPAKAAU na BBC

Keine Kommentare:

Kommentar veröffentlichen