Wamachinga wachachamaa Mwanza
Mjini Mwanza hali ilikuwa sio shwari ,kutokana na wamachinga kufanya vurugu wakidai kutotendewa haki
na halmashauri ya jiji hilo kwa kuhamishwa kutoka sehemu zao za kufanyia biashara pasipo kufuatwa
makubaliano
yaliyokuwa yamewekwa baina yao na halmashauri ya jiji la Mwanza.
Mabomu ya machozi na risasi yametumiwa na askari kuzima vurugu hizo,inasemekana watu watatu
wamepoteza maisha.
Wamachinga wakiwa wamechoma matairi katikati ya barabara za jiji hilo.
Hali ndio kama hivyo biashara zimesimama na watu wanatizama tu hali ilivyokuwa ikiendelea
Kamanda wa polisi mkoani mwanza Simon Sirro naye alikuwepo eneo la tukio
Keine Kommentare:
Kommentar veröffentlichen