Best Blogger TipsSoon

Donnerstag, 30. Juni 2011

TZMPAKAAU

Andy Cole  atoa kisomo  Makongo

andy cole, biography, legend
MSHAMBULIAJI wa zamani wa Manchester United na timu ya taifa ya Uingereza, Andy Cole amewataka vijana wanaochipukia katika soka nchini kuwa wasikivu kwa makocha
wao na kuzingatia mazoezi ili kufikia malengo yao.

Cole aliyeichezea klabu hiyo miaka 7 na kutwaa ubingwa mara 5, aliwasili nchini jana akitokea Kenya na baadaye kuzindua programu maalumu ya soka inayodhaminiwa na Kampuni ya simu za mkononi Airtel.


 

Programu hiyo inayofahamika kwa jina la Airtel Rising Stars inajumuisha Afrika nzima kutoa nafasi kwa wanasoka chipukizi na lengo lake ni kuibua na kuviendeleza kuanzia ngazi ya chini hadi taifa, ambapo wanafunzi watakaofanya vizuri watajifunza soka katika shule za soka, zinazomilikiwa na Man United.

Source:Majira,TZMPAKAAU

Keine Kommentare:

Kommentar veröffentlichen