Meneja masoko wa SEMES Atupele Elias akionyesha moja ya mashine za kufanyia usafi katika ofisi mbalimbali na numba mjini Arusha.
KAMPUNI ya Semes ya jijini la Arusha imeweka mikakati ya kuhakikisha kuwa inawaakomboa wanamke wa nchi ya Tanzania kwa kuwapa elimu ya ujasiriamali sanjari na kuwapatia mitaji ili iwawezeshe kujikwamua kiuchumi.Hayo yalisemwa na mkurugenzi wa kampuni hiyo Bw Elias Seme alipokuwa katika sherehe za kuzindua kikundi cha kampuni hiyo jijini Arusha.Alisema kuwa ili kuhakikisha kuwa wanawake wanaondokana na hali ya utegemezi kampuni hiyo imejipanga kuhakikisha kuwa wanawake wanapewa kipaumbele katika kuwakomboa kwa kuwapatia mitaji mbali mbali Bw Seme aliongeza kuwa
Baadhi ya wafanyakazi wa SEMES
SEMES imeshatoa mitaji ya shilingi milioni tano kwa mwaka huu ambapo pia wameweza kuanzisha vikoba kwa lengo la kukopeshana ili kuboresha maisha yao,Aliongeza kuwa mbali na hayo kampuni hiyo imefanikiwa kutoa ajira kwa vijana 21 ambapo lengo halisi ni kuweza kutoa ajira kwa watu 50-60 kwa mwaka .Akielezea changamoto inayoikabili kampuni hiyo alisema kuwa ni pamoja na ushindani wa kibiashara ambapo kumekuwepo na makampuni mengi kutoka nchi ya nje yanayohusiana na maswala ya usafi hivyo kuwepo na upinzani mkubwa.Alitaja mikakati waliyonayo kuwa ni pamoja na kuongeza vitega uchumi zaidi na kujiboresha ili iweze kujiongezea mapato zaidi ili kuwawezesha vijana wengi kujipatia ajira.
Vyanzo:TZMPAKAAU na Fullshangwe
Baadhi ya wafanyakazi wa SEMES
SEMES imeshatoa mitaji ya shilingi milioni tano kwa mwaka huu ambapo pia wameweza kuanzisha vikoba kwa lengo la kukopeshana ili kuboresha maisha yao,Aliongeza kuwa mbali na hayo kampuni hiyo imefanikiwa kutoa ajira kwa vijana 21 ambapo lengo halisi ni kuweza kutoa ajira kwa watu 50-60 kwa mwaka .Akielezea changamoto inayoikabili kampuni hiyo alisema kuwa ni pamoja na ushindani wa kibiashara ambapo kumekuwepo na makampuni mengi kutoka nchi ya nje yanayohusiana na maswala ya usafi hivyo kuwepo na upinzani mkubwa.Alitaja mikakati waliyonayo kuwa ni pamoja na kuongeza vitega uchumi zaidi na kujiboresha ili iweze kujiongezea mapato zaidi ili kuwawezesha vijana wengi kujipatia ajira.
Vyanzo:TZMPAKAAU na Fullshangwe
Keine Kommentare:
Kommentar veröffentlichen