Best Blogger TipsSoon

Donnerstag, 30. Juni 2011

TZMPAKAAU

Andy Cole  atoa kisomo  Makongo

andy cole, biography, legend
MSHAMBULIAJI wa zamani wa Manchester United na timu ya taifa ya Uingereza, Andy Cole amewataka vijana wanaochipukia katika soka nchini kuwa wasikivu kwa makocha
wao na kuzingatia mazoezi ili kufikia malengo yao.

Cole aliyeichezea klabu hiyo miaka 7 na kutwaa ubingwa mara 5, aliwasili nchini jana akitokea Kenya na baadaye kuzindua programu maalumu ya soka inayodhaminiwa na Kampuni ya simu za mkononi Airtel.


 

Programu hiyo inayofahamika kwa jina la Airtel Rising Stars inajumuisha Afrika nzima kutoa nafasi kwa wanasoka chipukizi na lengo lake ni kuibua na kuviendeleza kuanzia ngazi ya chini hadi taifa, ambapo wanafunzi watakaofanya vizuri watajifunza soka katika shule za soka, zinazomilikiwa na Man United.

Source:Majira,TZMPAKAAU

TZMPAKAAU

Oscar Kambona :Upande wa pili wa shilingi(2)

Na Maggid Mjengwa                                                                                  


-Ziara mbili za ughaibuni zilizovunja urafiki wa Nyerere na Kambona

Ahmad Rashid kiongozi aliyepita wa kambi ya upinzani

KUNA wakati nilimsikia Ahmad Rashid akitoa hoja bungeni. Wakati huo mbunge huyo wa CUF alikuwa kiongozi wa upinzani bungeni. Ahmad Rashid aliomba kambi ya upinzani bungeni ibadilishwe jina na badala yake iitwe kambi ya ushindani bungeni. Ni kwa vile neno ‘upinzani’ linatafsiriwa vibaya na wananchi.
Spika aliyepita wa bunge la Jamhuri ya Muungano Samwel Sitta

Spika Samwel Sitta alisimama na kutamka; “ Mtaendelea kuitwa hivyo hivyo kambi ya upinzani, kwa vile nyinyi ni watu wa kupingapinga tu!” Na maneno haya ya Samwel Sitta yanatokana na historia yetu. Maana, haya ni makosa ya kihistoria yaliyofanywa na waliojenga msingi wa taifa letu. Na ndio tunayoyaona hata katika mfarakano wa miaka hamsini iliyopita kati ya Julius Nyerere na Oscar Kambona.

Datei:Tz 1961.PNG
Bendera ya chama cha TANU



Na mara ile, mwaka 1965, TANU ilipoaachana na mfumo wa vyama vingi na kuasisi mfumo wa Chama kimoja Kambona alipata kutamka; ” Kwanini tupige marufuku ya vyama vingine vya siasa wakati tunajua wananchi walio wengi wanaipigia kura TANU?” Kambona akaongeza kusema; ” Bila shaka, umaarufu wa TANU utabaki kwa muda mrefu, lakini, je, pale umaarufu wa TANU utakapopungua, ina maana tuwe madikteta?” Alihoji Kambona.

Bendera ya TANU


Nimepata kukumbushia mara kadhaa, kuwa historia ni mwalimu mzuri. Na wanadamu hatupaswi kuwa vipofu wa historia yetu wenyewe. Kuifumbia macho historia yako ni kujiandalia njia ya kutumbukia korongoni, kwa kujitakia. Tunapoadhimisha miaka hamsini ya uhuru wa Tanganyika tuna lazima ya kuipitia na kuitafakari historia yetu. Kwa macho makavu na maangavu, tuangalie nyuma tulikotoka. Tuangalie tulipo sasa. Ndio, tufanye hivyo ili tuutafute mwelekeo mwema wa nchi yetu hata kwa miaka mingine hamsini ijayo.

Hayati Mwalimu Nyerere tar 9.12.1961

Naam. Julius na Oscar walikuwa viongozi vijana sana katika Tanganyika huru ya wakati huo. Ikumbukwe, wakati tukipata uhuru, Nyerere alikuwa na miaka 39 na Oscar alikuwa na miaka 36. Hawa walikuwa ni vijana waliokabidhiwa dhamana kubwa ya kuingoza nchi kubwa ya Tanganyika. Naamini, walikuwa ni wenye dhamira njema kwa taifa hili; Julius, Oscar, Rashid na wenzao wengine katika TANU.
Ukweli unabaki, kuwa Oscar Kambona hakuikimbia nchi yake kwa kashfa ya kuiba fedha ya Serikali au ufisadi mwingine. Na kwa utafiti mdogo tu niliofanya, nilichobaini, ni ukweli kuwa marafiki hawa wawili; Oscar na Julius walikuwa na mgongano wa tofauti ya kimaono ya kisiasa yaliyoathiri hata urafiki wao.
Hayati Oscar.S Kambona

Maana, haiyumkini Kambona aliyeaminiwa na Nyerere akaja kuwa Katibu Mkuu wa kwanza wa TANU, akawa Waziri wa kwanza wa Elimu wa Tanganyika huru, akaja kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani na hata kwa wakati mmoja kushika wizara mbili; Waziri wa Ulinzi na Waziri wa Mambo ya Nje. Kwamba, aje tena baadae kutuhumiwa uhaini na hata kushukiwa uraia wake.


Ndio, kwangu mimi, ya Kambona na Nyerere ilihusu zaidi mgongano wa tofauti za kimaono ya kisiasa . Na ukiingia kwa undani kwenye maandiko na simulizi utaupata ushahidi wa haya. Na kwa hakika, ili siasa ya nchi istawi, basi, inahitaji uwepo wa migongano ya kifikra. Hivyo basi, siasa ni migongano ya kifikra yenye kuhitaji majadiliano endelevu.


Tunaona, kuwa migongano ya kifikra kati ya Oscar na Julius ilianza kuonekana dhahiri katika ziara mbili walizozifanya kwa pamoja katika mataifa mawili tofauti. Ziara ya Marekani mwaka 1963 na ziara ya Uchina mwaka 1965. Na hapo katikati kuna jambo lililoopelekea uwepo wa mahusiano ya mashaka kati ya Julius na Oscar. Ni uasi wa jeshi wa Janauri 20, 1964.


Uasi ule ulipelekea Nyerere na Kawawa waende mafichoni, inasimuliwa walijihifadhi eneo la Kigamboni. Mjini alibaki Oscar Kambona aliyeshiriki kikamilifu kuwatuliza wanajeshi wale. Kimsingi, katika kipindi kile cha maasi, Kambona, kama angetaka, alikuwa na fursa ya kutwaa mamlaka ya nchi akisaidiwa na jeshi. Inasemwa, kuwa akiwa Waziri wa Ulinzi, Kambona alikubalika sana jeshini.

Mwl.Nyerere akiwa na mwenyekiti Mao("hii picha bado ipo katika kumbukumbu za chama cha kikomunist cha Uchina ambacho ndio chama tawala cha uchina hadi kesho")

Baada ya ziara ya Marekani akiwa na Oscar Kambona mwaka 1963 ambako Rais John Kennedy alimsifia sana Nyerere kwa kuonyesha uwezo wa kiungozi , miaka miwili baadae, mwaka 1965, Nyerere na msafara wake akiwamo Oscar Kambona walikwenda China kwa mara ya kwanza na kulakiwa na Mwenyekiti Mao Tse Tung. Nyerere akiwa kwenye gari la wazi na mwenyeji wake Mao , alishangiliwa na Wachina wapatao milioni moja waliojipanga barabarani.

Pale Ilala tulikoishi, nakumbuka nikiwa na umri wa miaka sita tu, usiku mmoja pale viwanja vya shule ya msingi Boma tuliangalia sinema ya ziara ya Julius Nyerere Uchina . Nyerere aliiona China na alivutiwa sana. ” What we have seen in China is relevant to us”. Nimemsikia Nyerere akiongea hayo kwenye kipande cha filamu ya zamani kilichopo mtandaoni . ” Ana maana, walichokiona China kinaweza kikafanyika kwetu. Na Julius alianza kwa kubadilisha hata staili yake ya mavazi, yakafanana na ya Mwenyekiti Mao, na wengine katika TANU wakamwiga.

Ni nini kilitokea kwenye Mkutano wa TANU wa Januari, mwaka 1967 na kabla ya hapo. Mkutano uliopelekea kumalizika kabisa kwa urafiki wa Nyerere na Kambona. Fuatilia toleo lijalo.




Tuna maswali mengi ya kujiuliza, moja kuu ni hili; Je, ni nchi ya namna gani tutayotaka kuijenga na hata kuvirithisha vizazi vijavyo? Kwa maneno mengine; ni jamii gani tunayotaka kuijenga? Sisi wa ’ Kizazi Cha Azimio’ tulikuwa wadogo sana katika miaka kumi ya mwanzo ya uhuru na hata utekelezaji wa Azimio la Arusha. Nimezaliwa Ilala, Dar es Salaam, Machi 11, 1966.


Ndio, kuna mema mengi tuliyoyaona, lakini, tukitafakari sasa, kuna mabaya mengi pia tuliyoyashuhudia. Tuna wajibu wa kusimulia mema na mabaya hayo kwa manufaa ya Watanzania wa kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Kati ya kumbukumbu zangu mbaya za wakati huo ni jinsi tulivyowaona wazazi wetu wakiishi kwa hofu. Waliogopa kushutumu mamlaka hadharani na kwa sauti. Waliishutumu Serikali na hata kiongozi mkuu wa nchi kwa kunong’ona. Wazazi wetu walimwogopa hata mjumbe wa nyumba kumi.

Ni ukweli, kuwa kwa wakati ule, Serikali na chama tawala havikuwa na uvumilivu wa sauti za upinzani.

Na siku zote, mamlaka bila upinzani huzaa kiburi na majigambo. Huzaa hali ya kutokujali na kukosa usikivu. Taratibu, huzaa hali ya kujisikia u-bwana mkubwa. Hali hii ikiachwa ikaendelea, basi, husababisha madhara makubwa kwa nchi. Huleta hasara kubwa kwa nchi, kiuchumi na kijamii.

Juma la jana nilimalizia kwa kuandika, kuwa makala haya ni jaribio la kuvunja ukimya wa juu ya nini kilitokea takribani miaka hamsini iliyopita. Ni mmoja tu wa mfano , wa jinsi umma ulivyofichwa ukweli wa juu ya nini hasa kilitokea kikasababisha mfarakano wa waliopata kuwa viongozi wa mstari wa mbele kwenye harakati za kuanzishwa kwa TANU na kudai uhuru wa Tanganyika; Julius Kambarage Nyerere na Oscar Salathiel Kambona.


Kuna aliyesoma makala yangu ya juma la jana na kuniuliza; ” Maggid, hivi wewe huogopi?” Ni kweli, kama ningeandika haya mwaka 1976 nilipokuwa mtoto wa umri wa miaka kumi tu, basi, vyombo vya dola vingenishukia mithili ya mwewe anayekishukia kifaranga cha kuku. Sio tu mimi ningeswekwa rumande ya watoto, bali hata mama na baba yangu wangetikiswa na dola kwa ’ dhambi’ ya kumzaa mtoto mwenye fikra za ’ kipinzanipinzani ’ na ’ kihainihaini’. Mtoto ’ anayepingapinga’ tu!


Na hapa ndipo kwenye moja ya mapungufu makubwa ya waliojenga msingi wa taifa letu; kuchukia wenye kufikiri tofauti na watawala. Na zaidi kuwachukia wenye ’ akili’ ya kufikiri na kuutumia vema welewa wao- hostility towards execelency. Si tunajua, kuwa utotoni tulisikia kuna maadui wa nchi wa aina mbili; maadui wa nje na wa ndani. Wapinzani ama wenye kufikiri tofauti ndimo walimowekwa wanaoitwa ’maadui wa ndani!’


Niseme tu, mfulilizo wa makala haya ni moja ya makala zangu muhimu tangu nianze kushika kalamu na kuandika makala magazetini. Na naandika nikiwa sina hata chembe ya hofu. Ni kwa sababu moja kuu; kuwa yanahusu historia yetu na mustakabali wa nchi yetu. Sote tuna wajibu wa kuandika historia yetu.


Hii ni nchi yetu. Hatuna sababu za kuionea aibu historia yetu, badala yake, tujivunie, kuwa tuna historia. Na ni unyonge na utumwa kusubiri wasomi kutoka Marekani na Ulaya waje kutafiti na kutuandikia historia yetu. Historia yako isimulie mwenyewe. Hivyo basi, tuna wajibu wa kuifanya kazi hiyo. historia itusaidie kutukumbusha machungu na furaha ya tuliyoyapitia kama taifa. Si kwa kuandika tu, hata kwa kusimulia machache tuliyoyashuhudia.


Niliahidi kuchambua zaidi juu ya marafiki hawa watatu; Kambona, Nyerere na Kawawa. Nitafanya hivyo sasa.

Mittwoch, 29. Juni 2011

TZMPAKAAU

Watanzania msibaguane kwa dini

Balozi wa U.S.A nchini Tanzania
Balozi wa Marekani nchini, Alphonso Lenhardt, amewataka Watanzania kuwa wamoja na kuachana na tabia ya kubaguana kwa misingi ya dini zao.
Lenhardt alitoa ushauri huo jana jijini Dar es Salaam katika ofisi za ubalozi huo alipokutana na baadhi ya viongozi wa dini.
Alisema dini ni kitu cha kuiweka jamii katika umoja na sio kuisambaratisha na kusema kuwa Tanzania imejaliwa kuwa na misingi imara ya watu kuheshimiana kupitia dini zao.

Chanzo:Ippmedia,TZMPAKAAU

Samstag, 25. Juni 2011

TZMPAKAAU

This week in pictures




Mama Michelle Obama ijumaa alipokuwa botswana alikaribishwa na ngoma Mama Michelle ametembelea klinik za watu wanaoishi na virusi vya ukimwi nchini botswana
Wa Syria bado wameendelea kushikilia msimamo wao hawamtaki Bashar Al Assad,lakini yeye anasema suluhisho ni kukaa na kumaliza tofauti zao.

Czech Slovakia wiki hii waliazimisha mwisho wa utawala wa Urusi baada ya vita vya pili vya dunia kwa kukipaka kifaru rangi hiyo.

Hii ni black hole mimi ,sina utaalamu zaidi ila unaweza ukatafuta taarifa zaidi kuwa hii ni nini hasa?

Wagiriki wiki hii walipiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu wao bw George Papandreou,kutokana na hali mbaya ya uchumi wa nchi hiyo.

Mafuriko makubwa yanaendelea nchini china,watu 130 wamepoteza maisha zaidi ya watu laki nane hawana makazi, watu zaidi ya 10,000,000 wamepoteza mali wameumia au wanateseka kutokana na kukosekana kwa huduma muhimu kama maji,umeme,chakula na miundo mbinu

Hizi ni kambi mpya za wakimbizi zilizoanzishwa nchini uturuki kuwahifadhi maelfu ya wakimbizi wanaotoka nchi jirani ya Syria
Huyu mtoto ana miaka nane anaitwa Raby akiwa mjini Wau southern Sudan kama mkimbizi kutoka jimbo linalogombewa la Abieyi wazazi wake wapo wapi,kaka zake,dada zake,anakula nini,analala wapi Mungu ndiye anayejua.

Benghazi vita imekuwa sehemu ya maisha,lakini ukiacha mzaha watu wengi sana wanapoteza maisha hali inatisha sana nchini Libya sasa kuna makaburi yasiyo na idadi,ukiachilia mbali uharibifu ambao hata wewe ni shahidi.
Waziri mkuu anayejua nini maana ya maisha....waziri mkuu wa Italia bw.Silvio Berlusconi ana kesi zinazomkabili,chama chake kimeshindwa mfululizo na wapinzani,hali ya uchumi ni mbaya hapa anakunywa Capuccino  katikati ya kikao cha serikali.


Komandoo wa Brazil akiwa mazoezini,Brazil ni nchi ambayo uchumi wake unakuwa kwa kasi, hivyo nchi hiyo kwa upande mwingine inajiimarisha zaidi na zaidi kijeshi kama zifanyavyo nchi kama China,India,Uturuki na nyenginezo

Wanamieleka wa kipakistani kama walivyokutwa na kamera katika mazoezi yao ya kila siku mchezo wa mieleka ya aina hii unahistoria ndefu nchini pakistani

Baada ya miaka kumi ya kupambana sasa ni muda wa kulala tu,hawa ni wanajeshi wa Canada nchini Afaghanistan jimbo la Kandhar wanajeshi wa Canada wanaondoka nchini Afghanistani mwezi ujao baada ya kupambana kwa zaidi ya miaka 10 na wataleban.

TZMPAKAAU

   Hörst Kholer ashangaa uharaka wa sarafu ya pamoja ya EAC
  • Ashauri maoni ya wananchi yasikilizwe na yazingatiwe
  • Asema EAC ijifunze toka EU(European Union) iliyochukua miaka 10 kuwa na Euro

Rais wa zamani wa ujerumani Hörst Kholer

Profesa Kohler aliyasema hayo, wiki iliyopita, mjini Arusha, kwenye mdahalo maalumuwa kuangalia Matarajio na Uhalisia wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) katika Ulimwengu wa Utandawazi. Mdahalo huo ulihudhuriwa na watu mbalimbali maarufu wakiwemo wanadiplomasia kadhaa.

Rais huyo wa zamani wa ujerumani ambaye pia ni mtaalamu wa uchumi na mwanasiasa wa Christlich Demokratische Union(CDU) cha ujerumani, ameeleza kushangazwa kwake na haraka inayoonekana katika kuzifanya nchi za Afrika Mashariki kuwa na sarafu ya pamoja. Amesema kwamba jambo hilo ni nyeti na linahitaji muda mrefu zaidi wa wananchi wanchi hizo kushauriana na kujadiliana kabla ya uamuzi wa kuwanayo haujafikiwa.

“Kwa nini kuna haraka katika jambo la msingi na muhimu kama hili?alihoji

 Proffesa Kholer anayasema haya wakati baadhi ya nchi wanachama wa E.U zikikabiliwa na matatizo makubwa kufuatia sarafu ya pamoja ya EURO nchi hizo ni kama Ugiriki,Spain na Ireland.

E.A.C(East African Community)

Kwa habari zaidi  http://www.raiamwema.co.tz/rais-wa-zamani-ujerumani-ashangaa-uharaka-wa-sarafu-ya-pamoja-eac

Donnerstag, 23. Juni 2011

TZMPAKAAU

Oscar Kambona :Upande wa pili wa shilingi

Na Maggid Mjengwa                                                                                  


”KAMBONA, ah, ah! Kambona, ameolewa, Wapi? Huko Ulaya! Wivu, wamkereketa!”



Oscar Salathieli Kambona




siku zote, wanadamu tunapaswa kufanya jitihada ya kuitafuta kweli. Tufanye hivyo ili tuyapate maarifa mapya. Wimbo huo hapo juu ni wa mchakamchaka. Uliimbwa na kaka na dada zetu mashuleni. Kuna wengi tuliousikia. Tukaamini, lakini kuna tuliojengewa kiu ya kutaka kujua ukweli wa jambo zima.

Naam. Mwaka huu tunaadhimisha miaka 50 ya Uhuru wetu. Na kwa mwanadamu, ili uweze kuyaelewa yanayotokea leo, na uweze kubashiri yatakayotokea kesho, basi, ni vema na ni busara ukajitahidi kuyajua yaliyotokea jana.


Kizazi cha sasa cha Watanzania kitapata maarifa mapya na hata kusaidiwa kuyaelewa yanayotokea leo kwa kukumbushwa na kusaidiwa kuyajua yaliyotokea jana. Maana; kuna waliojenga msingi wa nchi hii.
Mapungufu mengine tunayayaona leo yanatokana na makosa ya jana yaliyofanywa na waliojenga msingi wa nchi hii. Ni makosa ya kibinadamu.Ni mwanadamu gani asiyekosea?




Mwalimu Julius Nyerere mbele,nyuma ni Oscar Kambona

Tutafanya makosa kuadhimisha miaka hamsini ya uhuru wetu bila, japo kwa uchache, kujadili kilichowatokea marafiki hawa watatu na athari zake kwa Tanzania yetu ya leo.

Utabaki kuwa ni ukweli kuwa, kama Taifa, ya Kambarage, Kambona na Kawawa ni sehemu ya historia yetu . Maana; sio tu historia ya harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na hata kuanzishwa kwa TANU, bali historia ya nchi yetu haiwezi kukamilika bila, mathalan, kutajwa kwa jina hili: Oscar Kambona.

Lakini, kwa miaka hamsini sasa, ukweli juu ya nini kilichotokea mpaka Oscar Kambona akaikimbia nchi yake aliyozaliwa haujawekwa hadharani umma ukaelewa. Kwa Watanzania wengi, Oscar Kambona na kukimbia kwake nchi inabaki kuwa simulizi ya upande mmoja.
Na kwa vile shilingi ina pande mbili, hata ukichukia pande moja ya shilingi, si busara ukakaa na kuubondabonda upande unaouchukia. Bado ni shilingi yako.

Utotoni nimesikia simulizi za Oscar Kambona. Shuleni hatukusoma habari za Oscar Kambona na mchango wake katika kuanzishwa kwa TANU na ujenzi wa chama hicho na hata ushiriki wake katika harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.


Tuliosikia simulizi za Oscar Kambona tuliaminishwa kuwa, Kambona alikuwa msaliti kwa nchi yake. Kambona alikuwa bepari na alichukia Ujamaa. Kambona alikuwa mhaini na hata huko Ulaya alikokimbilia, alipanga njama za kumpindua rafiki yake wa zamani, Julius Nyerere. Naam, kulikukwa na simulizi nyingi mbaya juu ya Oscar Kambona.
Na katika dunia hii kuna wanaodhani wanajua, na kuna wale ambao wanajitahidi kujua. Nimechagua kuwa katika kundi hilo la pili; wanaojitahidi kujua.

Kazi hii ya kuutafuta ukweli hasa wa nini kilitokea miaka hamsini iliyopita, ni moja ya jitihada tunazopaswa kuzifanya wakati tukiwa hai; kujitahidi kujua.


Nimesikia simulizi za utotoni juu ya Oscar Kambona. Katika utu uzima wangu huu nimejitahidi kuyatafuta maandiko yenye kumhusu Kambona na wenzake wa enzi za Tanganyika.





Na hakika, kisa cha marafiki watatu; Kambarage, Kambona na Kawawa kinatoa somo muhimu kwa Watanzania wengi wa kizazi cha sasa.


[nyirenda-4.jpg]


Sio mbaya mtu ukijua mashujaa mbalimbali wa Tanzania. Pichani ni Hayati Baba wa taifa Mwl Nyerere akiwa na hayati  Major Alex Gweba Nyirenda  huyu ndiye shujaa aliyepandisha mwenge wa uhuru mlima kilimanjaro desemba tar 9,1961.


Nimejiridhisha kuwa Oscar Kambona alikuwa Mtanzania mzalendo wa nchi hii. Alitofautiana kimisimamo na rafiki yake Julius Nyerere juu ya namna ya kuendesha mambo katika Tanganyika huru, akaamua kuondoka yeye na familia yake.

Kilichofuata, ndani ya propaganda na uvumi ule dhidi ya Kambona kwa jinsi alivyoondoka, kulikuwa na ’ kimya kizito’. Ni kimya kilichodumu kwa nusu karne sasa. Ni kimya kwa vile hakukuwa na nafasi ya kusikia kutoka kwa Oscar kambona mwenyewe, jibu la swali hili muhimu; Kwanini Kambona aliondoka?

Na kulitafuta jibu la swali hilo kutatusaidia kuyaona makosa yaliyofanyika nyuma ili kuepuka kuyarudia tena. Maana, kimya kile cha miaka hamsini kwa namna moja au nyingine, kimesababisha kuyarudia baadhi ya makosa yaliyofanywa na waliojenga msingi wa taifa hili.

Tunajua leo, kuwa Kambona alitofautiana na Nyerere juu ya utekelezaji wa Azimio la Arusha. Alikuwa na mtazamo tofauti; hivyo basi, hakukuwa na dhambi ya kufikiri tofauti.

Kambona alihoji mantiki ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya chama kimoja bila upinzani wa kisiasa. Hakukuwa na dhambi ya kufikiri hivyo.

Tunaona sasa, msingi huo huo uliojengwa wa kuamini kuwa upinzani wa kisiasa ni uadui, ni dhambi, ndio kwa kiasi kikubwa umelifikisha taifa letu hapa lilipo.

Kwa nusu karne sasa, chini ya chama kimoja tawala, imejengeka misingi ya viongozi kulindana. Na fursa ilipopatikana, baadhi ya viongozi wetu wamekuwa matajiri wakubwa kwa njia haramu.

Tujiulize; Kambona alifanya dhambi gani kubwa kiasi cha kupata adhabu ile kubwa ya kukaa uhamishoni kwa miaka 25? Mandela alimzidi Kambona kwa mwaka mmoja katika ‘kutupwa gerezani’.

Na katika hili la Kambona na Nyerere kuna mengi ya kujiuliza: Hivi inawezekanaje marafiki wawili walioshibana wakafikia kufarakana kwa kiasi tulichokishuhudia? Ikukumbukwe, Nyerere na Kambona walikuwa marafiki kiasi cha Kambona kumfanya Nyerere kuwa ‘Mpambe wa Bwana Harusi’ kwenye harusi ya Kambona iliyofanyika London, Uingereza.








Ukiona hili jiwe la msingi linaloonekana kusahauliwa ujue umefika Tabora Boys a.k.a Kambini hii shule imefyatua viongozi wazuri sana kama huamini waulize wenzake Mwl Nyerere


Labda utajiuliza; urafiki wao ulianzaje? Nyerere alikutana na Oscar Kambona wakati Kambona alipokuwa shuleni Tabora mwishoni mwa miaka ya 40. Inasemwa kuwa Nyerere alimtangulia kiumri Oscar kwa kupishana miaka mitatu tu.
Kule Tabora Nyerere alikutana pia na Rashid Kawawa; naye alimzidi kiumri kwa miaka mitatu hivi. Hivyo basi, twaweza kusema kuwa urafiki wa Julius, Oscar na Rashid ulianzia Tabora, na harakati zao za pamoja za mapambano ya kisiasa zilianzia huko huko Tabora.
Julius Nyerere alikuwa Mkatoliki na hodari sana shuleni, akafika mpaka Uingereza kimasomo. Aliporudi akafanya kazi ya ualimu pale Pugu.

Alipoambiwa achague kati ya ualimu na siasa, Julius akachagua siasa.


Oscar naye alikuwa mwumini wa kanisa la Anglican na hodari sana shuleni. Naye akafika mpaka Uingereza kusomea sheria. Hakumaliza masomo yake, Nyerere alimshawishi akatishe masomo yake, arudi nyumbani kuimarisha TANU kwenye uchaguzi uliokuwa mbele yao.
Rashid Kawawa alikuwa Mwislamu. Alisoma mpaka Tabora, hakufika Uingereza, lakini akawa kiongozi mahiri wa vyama vya wafanyakazi . Katika TANU alikuwa ni mpiganaji wa kuaminika. Rashid alikuwa maarufu mjini. Alipata hata kucheza filamu maarufu ya ’ Mhogo Mchungu’.





Hayati Rahid Kawaka akiwa bado kijana



Rashid Kawawa hakuwa maarufu kama waziri mkuu tu lakini enzi za ujana wake alikuwa maarufu mji mzima


Rashid Kawawa kama mgeni rasmi miss Tanzania

Watatu hawa walikuwa marafiki, hilo halina shaka. Na baada ya Uhuru wa Tanganyika, Julius na Oscar walijenga nyumba zao pale kijijini Msasani kwenye pwani ya bahari. Naam. Walikuwa karibu sana kikazi na walichagua kuishi pamoja kama majirani.

Inasimuliwa kuwa nyakati za jioni, Oscar na Julius walipenda sana kutembea pamoja ufukweni pale Msasani wakijadiliana mambo mbalimbali. Bila shaka wake zao - Maria na Flora walitembeleana na hata ‘kuombana chumvi’.



Hayati mwalimu Kambarage Nyerere na mke wake Maria Nyerere

Lakini ilifika wakati Oscar na Julius hawakuonekana tena wakitembea pamoja ufukweni. Na pengine Maria na Flora hawakutembeleana na kuombana chumvi. Ikafika wakati pia Oscar na familia yake wakafungasha mizigo yao na kuondoka nchini kupitia Namanga. Nyumba yao ikaja kupata mpangaji mpya; Milton Obote, rafiki mwingine wa Julius Nyerere.

Oscar Kambona

Na mjini Dar es Salaam ukatawala uvumi zaidi kuliko ukweli wa kilichotokea. Ikasemwa kuwa Kambona ametoroka akiwa na sanduku limejaa pesa. Na pesa yetu wakati ule ilikuwa na thamani sana. Fikiri sasa kama sanduku la Kambona lilijaa manoti!


Na utotoni pale Ilala, nilipata kusikia uvumi kuwa huko Ulaya, Kambona amekuwa tajiri mkubwa. Wengine wakasema alishinda bahati nasibu. Wengine wakasema ni fedha alizotoroka nazo.

Na kuna wakati ukaenea uvumi kuwa kuna meli bandarini imezuiliwa kushusha shehena ya vitanda. Ni vitanda ambavyo Kambona alivituma Tanzania ili vitumike mahospitalini.

Kwa vile ukweli hasa kuhusu ugomvi wa Kambarage na Kambona haukupata kusemwa, basi, uvumi ukaendelea kusambazwa. Hivyo basi ’kimya kikuu’.
Makala haya ni jaribio la kuvunja ukimya wa juu ya nini kilitokea miaka hamsini iliyopita, na nini cha kujifunza.



Itaendelea.

TZMPAKAAU

 Lissu aja na hoja kama ile ya Kenya
  • Ni kuhusu kukatwa kodi katika posho za watumishi wa umma
  • Hoja yake yaibua kizaa zaa bungeni
  • Nimrodi Mkono,Wiliam Lukuvi ,George Simbachamweni,Jennista Muhagama na Peter Serukamba wote kutoka CCM waipinga hoja


Tundu lissu mwenye suti nyeusi akiwa amenyanyuliwa na mashabiki wake

 Lissu aliwasilisha mapendekezo ya kubadili muswada wa sheria ya fedha ya mwaka 2011/12 kwa kufuta kifungu kilichokuwa kinapendekeza posho zote wanazopewa watumishi wa serikali zisitozwe kodi, kwa kuwa ni kinyume cha mkakati wa serikali wa kuachana na matumzi makubwa yasiyokuwa ya msingi kama ilivyoanishwa katika mpango wa maendeleo wa miaka mitano.


Lissu alifafanua kuwa kuendelea kuwasamehe kodi ya mapato watumishi hao, ni sawa na kuzidi kuwaongezea walichonacho, na si kuwaangalia wale wa kipato cha chini kwa sababu watumishi wa chini hakuna anayelipwa posho inayofikia Sh. 100,000 ambacho ndicho kima cha kuanza kukatwa kodi kisheria.

Mmoja kati ya wapinzani wengi wa hoja hiyo Mbunge wa Kigoma mjini Peter Serukamba

Mbunge wa peramiho CCM Jenista Muhagama


Pandekezo la Lissu lilipingwa na wabunge kadhaa, akiwamo Jenista Muhagama (Peramiho- CCM), George Simbachaweni (Kibakwe-CCM), Nimrod Mkono (Musoma Vijijini - CCM), Peter Serukamba (Kigoma Mjini – CCM), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, wote wakipinga mapendekezo hayo.


Waziri wa Nchi  William Lukuvi



Tofauti na wenzake, Lukuvi alisema kuwa mawazo ya Lissu ni chanya kulingana na mpango wa maendeleo wa miaka mitano wa serikali, lakini ni vema kukawa na utaratibu mpana wa kuchambua makundi mbalimbali katika jamii na si kuibuka tu na msimamo wa kukurupuka kama ambavyo inapendekezwa na Lissu kwa sababu madhara yake yanaweza kuwa mabaya zaidi kwa watumishi wengine.

Nimrodi Mkono akiteta jambo na rais

Moto wa mabishano ulizidi kuwaka baada ya Mkono kusema kwamba mapendezo ya Lissu yangewaumiza madiwani ambao wanalipwa posho lakini hawana mishahara.

Zitto kabwe kulia kama anavyoonekana na mama yake bi Shida Salumu

Kutokana na kauli ya Mkono, mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, alisimama na kueleza kuwa kinachozungumzwa na baadhi ya wabunge kuwa msamaha huo wa kodi unawasadia watu wa kipato cha chini, wakiwamo walimu, madiwani, askari polisi na kada nyingine za chini, si za kweli kwa sababu katika kundi hilo hakuna anayelipwa posho ya Sh. 100,000 na zaidi kwani posho hii ndiyo inayopendekezwa ikatwe kodi.

Zitto alisema kuwa msamaha huo utawasaidia na kuwanufaisha zaidi wakubwa serikalini, wakiwamo mawaziri, makatibu wakuu na hata wabunge ambao tayari wana mapato makubwa wakilinganishwa na watumishi wengine.

Lissu alihitimisha hoja yake kwa kusema kuwa kimsingi hakuna ufanisi wowote utakaopatikana kwa kukataa kulipa kodi kwa kuwa wanaolengwa ni wakubwa ambao tayari wana mapato makubwa.

Vyanzo:TZMPAKAAU,IPPMEDIA

Dienstag, 21. Juni 2011

TZMPAKAAU

 R.O.M.A  na   Mechi za ugenini


  • Hapa hakuna kuremba ni mistari kwenda mbele

  • Kwa wapenda hard hip hop basi hii ngoma sio mbaya






Albino Fulani   naye  afanya   kweli

Wimbo wake unakwenda kwa jina la Usihofu  akishirikiana na msanii pipi

  • Flow zake zipo slow lakini zimepangwa zikapangika 
  •  Video yake  imekwenda shule kama sio chuo
Asa usiamini kila unachoambiwa prove by chekin this out

TZMPAKAAU

 Maskini Mzee Malecela


Mzee John Malecela na mpenzi wake bi Anne Kilango

John Samuel Malecela yupo taabani, amefanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo.
Spika wa Bunge la Jmhuri ya Muungano wa Tanzania, Anna Makinda aliwatangazia wabunge leo kabla ya kuahirisha kikao cha asubuhi kuwa Malecela ni mgonjwa.
Alisema, Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela haonekani bungeni kwa sababu Mzee Malecela ni mgonjwa.
Kilango ni mke wa ndoa wa mzee Malecela.
“Waheshimiwa wabunge kwa siku kadhaa mheshimiwa Anne Kilango haonekani, yupo anamuuguza mzee Malecela kwa sababu amefanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo,” alisema spika leo.
Hata hivyo, Spika Makinda hakueleza hali ya Malecela inaendeleaje, kama ana nafuu ama la.

Vyanzo:TZMPAKAAU,Global publishers

Samstag, 18. Juni 2011

TZMPAKAAU

   Do you know Malcom X?
  • Why his surname was X?
  • Who was he real?
  • And how  did he ended up.....?
It is claimed that he is the most influential African American who ever lived..........born in 1925 and died in 1939 his birth name was Malcom Little but he changed his surname afterwards and called himself Malcom X.He was an African American Muslim Minister,public speaker and human rights activitist.

To his admirers, he was a courageous advocate for the rights of African Americans, a man who indicted white America in the harshest terms for its crimes against black Americans.

His detractors accused him of preaching racism, black supremacy and violence. He has been called one of the greatest and most influential African Americans in history, and in 1998, Time  named The autobiograpy of Malcom X as one of the ten most influential nonfiction books of the 20th century.



Why Malcom Little  refused his surname ?




What was Malcom's Ambition?


 Malcom X who has been to jail later coached by prophet Elijah Mohamed led the movement toward demanding total  equality,justice and rights of  the African American those  times called Negroes, he was a muslim at the back ground but at the fore ground he claimed himself every now and then as a Negro.
 This is his longest speech


Malcom X was agressive at demanding the rights and he spoke direct without any hesitation
here speaking about traitors


                                   

 Anyone who defends the rights of the poor against the oppresions of the powerful ones  doesnot have the nice end he Malcom X was shot and died in Newyork at the time he was about to deliver his speech he died at the age of 39.


Malcom X longest speech





Sources :Wikipedia,BBC,Youtube,TZMPAKAAU

TZMPAKAAU

Spika wa bunge sasa ashtakiwa
  • Ni kwaajili ya upendeleo na upindishaji wa kanuni  kwa makusudi

Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imemshtaki Spika wa Bunge, Anne Makinda, kwa kamati ya Kudumu ya Kanuni za Bunge, kwa madai kuwa anapindisha kwa makusudi kanuni za Bunge ili kuwakandamiza wapinzani na kuwapendelea mawaziri na wabunge wa CCM.

Spika wa bunge la Tanzania Anna Makinda

Msimamo huo ulitaangazwa jana na Mnadhimu Mkuu wa kambi hiyo, Tundu Lissu, ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), kwa waaandishi wa habari mjini Dodoma

Mbunge wa Singida Mashariki(CHADEMA) Tundu Lissu

Alisema Spika anazijua vyema akanuni za Bunge kwa kuwa amekaa bungeni kwa zaidi ya miaka 30 na amekuwa Naibu Spika kwa miaka mitano, lakini anapoona maslahi ya chama chake yanaguswa amekuwa kwa makusudi akipindisha kanuni kuwabana wapinzani.

Alitoa mfano jinsi Spika alivyokataa Waziri Mkuu asijibu swali lake katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo juzi, akidai kuwa suala hilo liko mahakamani na haliwezi kujadiliwa na Bunge kwani kufanya hivyo ni kuingilia mhimili mwingine wa mahakama.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda na mke wake bi Tunu Pinda

Lissu alimuuliza Pinda kama imekuwa sera ya serikali ya Tanzania kuua raia wake na wahusika kutochukuliwa hatua zozote kwani wananchi wanaozunguka mgodi wa North Mara wamekuwa wakiuawa na polisi na walinzi wa mgodi huo bila kuchukuliwa hatua.

“Spika alikataa swali langu lisijibiwe kwa madai kwamba suala hilo liko mahakamani na alipoombwa mwongozo wake kutokana na ukweli kwamba hakuna kesi hata moja ambayo imefunguliwa au inayoendelea katika mahakama yoyote ya Tanzania inayohusu mauaji ya wananchi wa Nyamongo au yanayowahusu polisi wanaohusika na mauajai hayo, Spika alidai kwamba wauliza maswali wenyewe walikuwa wakikabiliwa na mashtaka ya jinai katika mahakama ya wilaya ya Tarime yanayotokana na matukio ya mauaji ya watu watano yaliyofanywa na polisi kwenye mgodi huo,”alisema.


“Ukweli ni kwamba mimi sina kesi inayohusiana na mauaji ya Nyamongo, mimi na wenzangu tumeshtakiwa kwa kuingia kijinai katika eneo la kuhifadhia maiti hospitali ya wilaya ya Tarime, kufanya mkusanyiko haramu na kuwazuia mganga wa hospitali hiyo na askari polisi kufanya uchunguzi wa miili ya marehemu, sasa kesi hiyo inahusiana vipi na swali langu la mauaji ya Nyamongo kama sio kumkingia kifua Waziri Mkuu?” alihoji.
Alisema suala la mauaji ya Nyamongo halijawahi kufikishwa mahakamani hivyo kukataa swali lake lisijibiwe ni kuikinga serikali isiwajibike kwa makosa ya mauaji dhidi ya raia ambayo imekuwa kawaida.
Alisema inawezekana Spika alitoa msimamo huo bila kupewa maelezo sahihi kuhusu mauaji ya Nyamongo.



Spika wa sasa wa bunge  Anna Makinda

“Spika anakula kiapo cha kufanyakazi kwa kufuata kanuni na bila upendeleo, sasa na si mara ya kwanza anaonekana kwenda kinyume cha kiapo chake cha kufanya kazi bila upendeleo, kwa kuwa uamuzi wa Spika sio wa mwisho na kanuni zinaturuhusu kumshtaki tunampeleka kwenye kamati ili imchunguze na kutoa majibu ya suala hili haraka iwezekanavyo.

“Tulisita sana kuchukua uamuzi huu wa kumshtaki, lakini tumeona tukiacha mambo haya yataendelee na Spika atakuwa dikteta na mijadala muhimu itazimwa kila siku, barua ya malalamiko tumeshaikamilisha na leo tunaiwasilisha kwa kamati husika,”alisema Lissu.
Lissu alisema kwa kuwa malalamiko hayo yanamhusu mwenyekiti 

Vyanzo: TZMPAKAAU,Ippmedia.


Donnerstag, 16. Juni 2011

TZMPAKAAU

Atakaye kalia kiti alichokiacha Osama  ni huyu
  •  Wamarekani waahidi kumkamata na kumuua
  •  Donge nono kutolewa kwa atakayesababisha kukamatwa kwake ni bilioni 37 za Tanzania(25million$)
  • Jamaa ni raia wa Egypt
  •  Baba na mama yake walikuwa madaktari
  • Yeye ana stashahada ya udaktari wa macho
Osama Bin Laden (left) and Ayman al-Zawahiri (file photo)
Kushoto ni aliyekuwa kiongozi wa Al Qaeda Osama na kulia ni Ayman Al zawahiri.
Ayman al-Zawahiri, ambaye kwa muda mrefu mno amekuwa msaidizi wa Osama Bin Laden katika kuiongoza Al-Qaeda, na akishikilia nafasi ya pili katika kutoa amri, sasa ataliongoza kundi hilo.
Hayo ni kwa mujibu wa taarifa katika wavuti ya kundi hilo.
Ayman al-Zawahiri
Kiongozi mpya wa kundi la Al-Qaeda
Kundi la Al-Qaeda limeonya kwamba litaendelea na vita vyake dhidi ya Marekani na Israel chini ya uongozi wa Zawahiri.

Wadadisi wa masuala ya Al-Qaeda wanaelezea kwamba Zawahiri, mwenye umri wa miaka 59, na aliyezaliwa nchini Misri, ni mtu mwerevu sana, lakini hana uwezo wa kuwavutia wafuasi wengi kama alivyofanya Osama.

Baadhi ya wadadisi wanasema yeye ndiye aliyepanga na kuendesha shughuli nyingi zilizohusiana na shambulio la Marekani la 9/11.

Na haya ni maneno yake katika video aliyotolewa na Al Qaeda mwezi huu

"We must continue on [Bin Laden's] path of jihad to expel the invaders from the land of Muslims and to purify it from injustice.
The man who terrified America in his life will continue to terrify it after his death. You will continue to be troubled by his famous vow: You shall not dream of security until we enjoy it and until you depart the Muslims' lands.
America is not facing an individual or a group, but a rebelling nation, which has awoken from its sleep in a jihadist renaissance."

Source:BBC,TZMPAKAAU

TZMPAKAAU

 Je wajua kwamba wajerumani walifanya nini katika mfumo wetu wa elimu?


   Do you know that the Germans made small but a solid foundation to Tanzanian education system?
  • Je wajua shule ya kwanza ya sekondari ni Tanga Tech
  • Unajua kiswahili ilikuwa ndiyo lugha ya kufundishia
  • Je wajua wajerumani hawakuwasomesha wanawake

Hii bendera ilionesha eneo walilotawala wajerumani
German empire flag




 You wanna know  more read this!!!


In the 20 years preceding World War I, Germany created a three-tiered system of education. There were 60 nebenschulen (primary schools), which offered 3 years of courses in reading, writing, and arithmetic; there were also 9 hauptschulen that offered 2 additional years of vocational training. Germany built one oberschule or high school in Tanga, which offered clerical, industrial, and teacher training, as well as some academic courses. At its zenith, the high school had 500 students and 4 German teachers on its staff.


Swahili was the language of instruction, German was offered as a foreign language. Missionaries Although were also encouraged to create schools for the indigenous population. By 1900, there were 600 missionary schools with a combined enrollment of over 50,000 students. In 1914, more than 95 percent of students enrolled in Tanganyika's schools were in mission schools. The number of schools had grown to over 1,000, and total enrollment climbed to 150,000 students. Government schools aimed to produce clerks, tax collectors, interpreters, artisans, and craftsmen, while missionaries aimed to produce westernized Christian converts, alienated from their own traditional culture. Since missionaries educated most Africans, it is not surprising that at independence many were hostile to traditional chiefs. Missionary schools were uncompromising spearheads of Westernization.

Hii ni MV Liemba ilitengenezwa na wajerumani kipindi cha vita ya kwanza Kigoma Tanzania na baadaye baada ya kushindwa vita wajerumani wakaizamisha,kipindi cha utawala wa waingereza  wakaitengeneza meli imetumika kwenye filamu ya Queen of africa na  sasa inapiga safari za Mpulungu Kigoma


(During WW1 the Germans sent the 1300 ton steamship "Graf von Goetzen" in pieces by train from Dar es Salaam to Kigoma. She was assembled there, but sunk in Lake Tanganyika by the Germans themselves as defeat became apparent. She was salvaged by the British in 1924, renamed the "Liemba" and (allegedly) starred as the German destroyer in the film "The African Queen" before taking up service as the ferry up Lake Tanganyika. She now sails from Mpulungu to Kigoma and back once a week.)




The German system did not educate girls because Western education began along the Muslim Coast where custom dictated that girls not be educated. It emphasized submissiveness, not enlightenment, in women.
This educational system laid a firm foundation for a national language, Kiswahili, and secular education. German administrators often corresponded in Swahili. The Germans laid a small but solid foundation for Tanzania's educational system. In 1903 there were 8 government schools and 15 mission schools. No statistics are available on the number of students in 1903. By 1911 the German colonial government had built 83 schools, while missionaries built 918 schools in Tanganyika. Government schools had 3,192 students, while missionary schools taught 63,455 students. In 1914, there were 99 German colonial government sponsored schools. By contrast, missionaries had constructed 1,852 schools. Government schools educated 6,100 students, but missionary schools educated an amazing 155,287. Clearly, missionaries educated the overwhelming majority of Tanganyikan pupils during the German colonial era.



Watu mnasikia "Hela " hamuwaulizi wababu wa enzi hizo kwanini hela hilo jina limetoka wapi,Enzi za wajerumani sarafu iliyokuwa inatumika ilikuwa inaitwa "Heller" na hii sarafu ilitumika Tanganyika Ujerumani na Austria enzi hizo......na maana ya "Heller" ni inayog'aa
(Heller was the old Austrian and Germany coin used as a legal standard of exchange of goods or services)


The German system of education put emphasis on practical education and health improvement. When England took over, they were impressed by the standard of literacy reached by Tanzanian Africans, especially those who had had the opportunity to study science and math in Germany. They produced skilled workers for the German colonial enterprise. Their schools were less like the German gymnasiums, which emphasized Latin and classical learning, and more like the German Volksschule, which were geared to the general public. The British adopted the German policy of cooperation with mission schools in the fight against illiteracy.



Mwanza "Rock City" lakini huu mwamba unaitambulisha Mwanza kuliko kitu chochote na hili jiwe linaitwa Bismark rock kama kumbukumbu kwamba wajerumani waliitawala Tanganyika kipindi fulani na Otto von Bismark ndiye alikuwa Chancellor wa ujerumani kipindi hicho.
(Bismark rock Mwanza marks the Germans colonial era in Tanganyika until tommorow)
All education stopped in Tanzania during World War I. With Germany's defeat, the victors divided the territory between Portugal, Belgium, and Britain. Britain administered what came to be known as Tanganyika, a trust territory, under a League of Nations mandate. Britain's stated educational purpose in 1920 was to develop the people, as far as possible, on their own lines and in accordance with their own values and customs. Britain allowed missionaries to play a major role in education and subsidized schools, which gave them greater control over the curriculum. The Universities Mission to Central Africa (UMCA) schools were Anglican and very British. Anglican schools had the biggest single influence on Tanzanian education during the British era. Despite this, over 80 percent of mission schools were foreign, non-British. This presented a security problem after 1926 when the League of Nations readmitted Germany, and German missionaries returned to teach in Tanzania.


Source:Stateuniversity.com,TZMPAKAAU